The government is now operating in accordance with the Guidance on Caretaker Conventions, pending the outcome of the 2025 federal election.

COVID Ndefu

Watu wengi wanaougua COVID-19 hupona kabisa ndani ya wiki chache za dalili za kwanza. Hata hivyo, watu wengine wanaweza kupata madhara ya muda mrefu kutokana na maambukizi yao. Pata maelezo juu ya COVID ndefu na mahali unapoweza kupata msaada kwa dalili zako zinazoendelea.

Kuhusu COVID ndefu

Neno 'COVID ndefu' hutumiwa kwa kawaida kuelezea zote mbili:

  • COVID-19 zenye dalili zinazoendelea - dalili za COVID-19 zinadumu zaidi ya wiki 4
  • hali/ugonjwa baada ya COVID-19 - dalili za COVID-19 baada ya wiki 12 ambazo hazijaelezewa na utambuzi mbadala.

COVID ndefu inaweza kujitokeza kwa njia tofauti kwa watu tofauti na dalili zinaweza kuwa ndogo hadi mbaya.

Dalili za COVID Ndefu

Dalili za kawaida zinazoripotiwa na COVID ndefu ni:

  • uchovu (kuchoka)
  • upungufu wa pumzi
  • matatizo na kumbukumbu yako na makini ('ukungu wa ubongo').

Dalili zingine ni pamoja na:

  • mapigo ya moyo, maumivu ya kifua au kubana kwa kifua
  • kikohozi
  • mabadiliko katika ladha au harufu
  • maumivu ya viungo na misuli
  • kuhisi pini na sindano
  • matatizo ya kulala (kukosa usingizi)
  • mabadiliko ya mhemko (kuongezeka kwa wasiwasi, hangaiko au unyogovu)
  • kizunguzungu
  • kichwa kuuma
  • homa ya kiwango cha chini
  • upele wa ngozi, upotezaji wa nywele
  • kichefuchefu, kuhara, maumivu ya tumbo, kupoteza hamu ya kula.

Katika watoto, dalili ni pamoja na:

  • dalili za hisia
  • uchovu
  • matatizo ya kulala.

Sababu za hatari kwa COVID ndefu

COVID ndefu inawezekana zaidi kutokea katika watu ambao:

  • hawajachanjwa
  • walikuwa na ugonjwa mbaya wa COVID-19, pamoja na wale ambao waliolazwa hospitalini au walihitaji utunzaji mkubwa
  • walikuwa na hali au ugonjwa wa msingi kabla ya COVID-19, kama vile shinikizo la damu, ugonjwa sugu wa mapafu, ugonjwa wa kisukari na fetma.

Kupata matibabu kwa COVID ndefu

Ikiwa una wasiwasi kuhusu dalili zinazoendelea baada ya uliugua COVID-19, unapaswa kuwasiliana na daktari wako kwa ukaguzi wa matibabu.

Hakuna kipimo kwa COVID ndefu. Daktari wako atauliza kuhusu dalili zako na athari zao kwenye maisha yako. Anaweza kupendekeza vipimo kadhaa ili kutambua sababu zinazowezekana za dalili zako na kuondoa hali zingine kuwa sababu.

Hakuna tiba moja au dawa moja ya kutibu COVID ndefu. Daktari wako atazungumza nawe kuhusu utunzaji na msaada unaoweza kuhitaji. Anaweza kukupa ushauri kuhusu:

  • kufuatilia na kusimamia dalili zako nyumbani, kama vile kutumia shajara ya dalili
  • dalili zinazoweza kuhitaji huduma ya matibabu (kama vile dalili mpya au zinazozidi kuwa mbaya) na mahali pa kutafuta huduma ikiwa unapata dalili hizi
  • nini cha kutarajia katika wiki na miezi inayofuata kuugua COVID-19
  • misaada kwa hatua za mtindo wa maisha, kama vile lishe, shughuli za kimwili na ushauri nasaha.

Ikiwa dalili zinaathiri sana maisha yako, unaweza kuelekezwa kwa daktari bingwa au huduma ya urekebishaji inayoweza kukusaidia kudhibiti dalili zako na kukusaidia kupona.

Kupona kutoka COVID ndefu

Nyakati za kupona zitatofautiana kwa kila mtu na dalili zako zinaweza kutofautiana kwa muda. Watu wengi watapata nafuu katika miezi 3 hadi 4. Hata hivyo, kwa watu wengine, dalili zinaweza kudumu kwa muda mrefu zaidi.

Kujizuia dhidi ya COVID ndefu

Njia bora zaidi ya kuzuia COVID ndefu ni kujikinga dhidi ya kuambukizwa.

Kusasisha na chanjo zako za COVID-19 kunaweza kusaidia kuzuia maambukizi ya COVID-19 na kukulinda dhidi ya kuwa mgonjwa sana. Watu ambao wanaochanjwa wana uwezekano mdogo wa kuripoti COVID ndefu ikilingana na watu ambao hawajachanjwa.

Majibu ya serikali

Kufuatia mwelekezo wa tarehe 1 Septemba 2022 kutoka kwa Waziri wa Afya na Utunzaji wa Wazee, Mheshimiwa Mbunge Mark Butler , Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya, Utunzaji wa Wazee na Michezo ilihoji na itaripoti kuhusu COVID-19 ndefu na maambukizi ya COVID-19 ya mara kwa mara.

Soma ripoti ya muda.

Habari zaidi

Date last updated:

Help us improve health.gov.au

If you would like a response please use the enquiries form instead.